Kampuni ya UDA-RT inautaarifu umma kuwa huduma za mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, imesitisha huduma zake kati ya Kimara - Kivukoni, Kimara - Gerezani, Morroco - Kivukoni na Morroco - Gerezani kuanzia saa 10: 30 alfajiri leo Jumatatu Mei 13, 2019, kufuatia kujaa maji katika eneo la Jangwani.

Huduma zinazotolewa sasa ni kati ya Kimara - Mbezi, Kimara - Magomeni Mapipa, Kimara - Morroco, Gerezani - Muhimbili, Kivukoni - Muhimbili na Gerezani - Kivukoni.

Tunaendelea kufuatilia hali ya maji katika eneo husika, maji yakipungua huduma zitarejea katika hali ya kawaida. Tunaomba radhi kwa usumbufu unatokana na kusitishwa kwa safari hizo.

Deus Bugaywa
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano UDA-RT.