Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limetoa taarifa kuwa sikukuu ya Eid El Fitr itakuwa siku ya Jumatano, Juni 5 au Alhamisi, Juni 6, kutegemeana na kuandama kwa mwezi.

Sherehe za Eid El Fitr kitaifa kwa mwaka 2019 itafanyika mkoani Tanga, ambapo swala ya Eid itafanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa uliopoa barabara ya 10 ngamiani Tanga mjini kuanzia saa 1:30 asubuhi.

Baraza la Eid litafanyika katika ukumbi wa Tanga Beach Resort, ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Soma taarifa nzima ya BAKWATA kuhusiana na sikukuu ya Eid hapa chini.