Mkuu wa shirika hilo ametoa taarifa hiyo leo akiongeza kusema kwamba uamuzi wa mwisho kuhusu suala hilo utatolewa na wasimamizi wa kampuni hiyo. Ndege za Boeing 737 Max zilizuiwa kuruka duniani mwezi Machi baada ya kutokea ajali mbaya nchini Ethiopia iliyouwa watu wote 157 waliokuwa ndani ya ndege hiyo, ambapo ilikuwa ni ajali ya pili kubwa katika kipindi cha miezi mitano kusababishwa na aina hiyo ya ndege ya Boeing.