Mwanaume mmoja raia wa Japan, amepoteza maisha ndani ya Ndege akitokea Mexico City baada ya kumeza kete 246 za Cocaine.



Ndege hiyo, iliyokuwa ikielekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Narita nchini Japan ililazimika kutua kwa dharura katika jimbo la Sonora nchini Mexico mwanaume huyo alipoanza kupoteza fahamu.

Mamlaka zimesema mtu huyo aliyejulikana kwa jina la Udo N, alipoteza maisha baada ya ubongo wake kujaa maji kutokana na matumizi ya madawa kupita kiasi.

Kwa mujibu wa taarifa ya mwanasheria mkuu wa jimbo la Sonora, Kete zilizokua na urefu wa sentimita 2.5 na upana wa sentimita 1 zilikutwa tumboni na kwenye utumbo wakati wa uchunguzi.


54 people are talking about this
Twitter Ads info and privacy
Kwa mujibu wa shirika la habarila BBC, Abiria wengine 198 waliobaki waliendelea na safari baada ya kutua kwa dharura katika mji wa Hermosillo. Mamlaka za Mexico zimesema zitaendelea na uchunguzi.