Wema: Nitazaa na Idris

LICHA ya madai kuwa wapenzi wawili, Idris Sultan na Wema Sepetu wamemwagana, muigizaji huyo nyota na Miss Tanzania 2006, amesema anataka kuzaa na mshindi huyo wa Big Brother Hotshots 2014 kutokana na jinsi anavyojali na mwenye huruma nyingi.
Akiteta na gazeti la Amani hivi karibuni, Wema alisema atajisikia fahari sana endapo mtoto wake wa kwanza angezaa na Idris kwa kuwa amemuonesha dhahiri kuwa ni baba bora.

“Kiukweli namuomba sana Mungu kila kukicha, baba wa mtoto wangu awe ni Idris kwa kuwa ni mwanaume pekee ambaye naona ni mwenye mapenzi ya dhati kwangu,” alisema Wema