Video ya aibu inayomuonesha msanii maarufu wa filamu Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ akicheza kihasara mbele ya mwanaume imevuja, Risasi Jumamosi linayo kibindoni.

‘Klipu’ hiyo ambayo Wema anaonekana akikata mauno huku suruali aliyokuwa amevaa ikimvuka na kuacha wazi sehemu ya makalio yake, ilivujishwa hivi karibuni na mdau mmoja wa burudani ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.

“Hii video niliichukua siku ya ile eventi ya Christian Bella ya kutimiza miaka 10 pale Escape One. Wakati akicheza na msanii wa Kundi la Pah One aitwaye Igwe, Wema alionekana kama alikuwa amelewa, alikuwa akikata mauno lakini aibu zaidi ilikuwa pale ambapo ile suruali yake ilipomvuka na sehemu ya makalio yake kubaki wazi.


“Sidhani kama alikuwa kavaa kufuli, baadhi ya watu waliokuwa wakimkodolea macho walishindwa kuamini kama ni Wema yule wanayemjua,” alisema mnyetishaji huyo.
Baada ya mwandishi wetu kupata nafasi ya kuiangalia mwanzo mpaka mwisho, alijiridhisha kuwa aliyekuwa akionekana kwenye video hiyo ni Wema na kweli alichokuwa akifanya ni aibu tupu.

Aibu yake ni pale ambapo suruali inamvuka na kuacha sehemu zake za siri wazi lakini pia staili ya kumkatikia msanii aliyekuwa akicheza naye kwani jamaa alikuwa ‘akikamatia chini’ huku naye akionekana kutokwa na udenda.

Paparazi wetu alijaribu kumtafuta Wema ili kuizungumzia ‘klipu’ hiyo lakini simu yake kila ilipopigwa ilikuwa haipokelewi.

Chanzo:GPL